Breaking News

NYOTA NDOGO AJAPENDEZWA NA MAMBO YA MUSTAFA NA HUDDAH, HAYA NDIYO MADONGO YAKE.





Drama ya uhusiano kati ya Huddah Monroe na rapper Colonel Mustafa wa Kenya inazidi kuwa kubwa baada ya muimbaji wa Mombasa, Nyota Ndogo naye kuingia kwenye picha. Nyoto Ndogo amempa makavu live rapper huyo wa Ogopa Deejays kuwa anachokifanya kinamshushia hadhi yake.

“Unayoyafanya unafikiria kuitwa baba kesho? maana ni upuuzi mtupu,” Nyota Ndogo amemchana Mustafa. “Umri wako hauambatani na vituko unavyo vifanya kwahivyo rudi nyuma ubadilishe. shame on you. wewe hufai kuitwa kioo.Umeshindwa kuandika nyimbo? kwaivyo unaona bora utafute visangaa? vinakupa sifa but unapata nini zaidi ya sifa hizo? hela kitandani?”

“Huyu mustafa hafai kuitwa kioo chajamii kabisa, umri wake na vituko vyake tafauti kabisa.uzee unaingia bado afanya mambo ya kitoto.shame,” aliongeza.

Mustafa na Huddah wameendelea kulianika penzi lao hadharani na hivi karibuni wataachia wimbo wao. “Can’t wait for my Song with @Mustafa_254 to land these streets . It was a first for me . But in life everything is possible,” alitweet Nyota Ndogo.
Asante kwa kutembelea Mwinyi Blog, naomba ubonyeze HAPA ulike page yangu ya facebook ili uendelee kupata matukio mbalimbali ya hapa na pale.